MOHAMED SALAH KUJUMUISHWA KWENYE BALLON DO'R,JE UNAJUA NI KWANN ATASHINDA MWAKA HUU?VIGEZO HIVI HAPA
Hakuna kitu kinachotafuna nyoyo za watu kama chuki na unafiki. Walio wengi hawapendi ukweli wa kile wasichokipenda uzidi kudumu. Tukiachilia ushabiki wetu na unazi tulio nao Mo Salah amekuwa na msimu bora kuzidi mchezaji yoyote ndani ya EPL.
Ametwa tuzo ya mchezaji bora wa mwezi mara 3 na hii inadhihirisha wazi kuwa DALILI YA MVUA NI MAWINGU. Najua roho zinawauma hasa ndugu zangu upande wa pili wanaotokea mashariki mwa Jiji la Liverpool wakipitia mji wa Warrington umbali wa kilometa kama 50 sawa na maili 31 na wale vibaraka wa Mrusi waliomtelekeza. Enewei

Kinachonisikitisha zaidi ni kuamini kuwa mchezaji bora lazima timu yake ipate mafanikio. Huu ni uchuro ambao Sepp Blatter ataulizwa na malaika wa Michezo mbinguni. Walio wengi wanaamini ili ubebe Tuzo ya Mchezaji bora wa Dunia lazima timu yako itwae Makombe makubwa kama UCL. Wanasahau Rivaldo alibeba tuzo hiyo na kumwacha nje Andy Cole na Dwight York na Beckham waliobeba makombe manne kwa msimu.

Ronaldo ni mmoja kati mchezaji bora kabisa wa muda wote. Najua mshindani mkubwa wa Salah ni Ronaldo. Ronaldo hana cha kupoteza. Najua anatamani Ballon D Or ya 6 ili kumpoteza mpinzani wake. Lakini nafsi yangu inaamini sio jipya kwake. Tayari tunaamini ni bora. Ballon D or 6 haiwezi kubadili chochote wala haiwezi kumfanya mashabiki wa Messi wampende. Kwa Ronaldo na Messi inatosha mazee. Au mnaonaje? Achukue mwingine sasa? Soka sio lao tu. Wakaushe tu

Comments
Post a Comment